Who was the first man made?
Adam
The Final War
Armageddon
How old was jesus when he was anointed?
29 years old
Defeated Goliath
David
How old was Abraham when God Asked him to leave his homeland?
75 yrs
How old was Abraham when he had Issacc
100
What message will we proclaim in the great tribulation?
A message of dread
Je, nyoka aliyezungumza na Hawa alikuwa na miguu?
Zaidi ya hilo, kama vile nyoka halisi anavyoweza kuumiza kisigino cha mtu, Shetani akiwa katika hali yake ya kushushwa ‘angetia jeraha kisigino’ cha “uzao” wa Mungu. (Mwanzo 3:15) Yesu Kristo ndiye sehemu kuu ya uzao huo, naye aliteseka kwa muda mfupi mikononi mwa watumishi wa Shetani. Lakini mwishowe, Kristo na waandamani wake Wakristo watiwa-mafuta ambao wamefufuliwa, wataponda kabisa kichwa cha nyoka huyo wa mfano. (Waroma 16:20) Hivyo, laana ya Mungu kuelekea nyoka anayeonekana ilifananisha hali ya kushushwa na kuharibiwa kabisa kwa “nyoka wa zamani” asiyeonekana, Shetani Ibilisi.
Wakati wa kuzingirwa na kuharibiwa kwa Yerusalemu, Ezekieli alikuwa “bubu” katika njia gani?
Je, Ezekieli alikuwa bubu kihalisi wakati huo? Bila shaka sivyo, kwa sababu hata baada ya “ububu” huo, alitoa unabii ulioelekezwa hasa kwenye nchi jirani ambazo zilishangilia kuanguka kwa Yerusalemu. (Ezekieli, sura za 25-32) Mapema katika kazi ya Ezekieli akiwa nabii na mlinzi, Yehova alikuwa amemwambia: “Nitaufanya ulimi wako ushikamane na kaakaa la kinywa chako, nawe hakika utakuwa bubu, na kwao wewe hutakuwa mtu mwenye kutoa karipio, kwa sababu wao ni nyumba yenye kuasi. Nami ninaposema nawe, nitakifungua kinywa chako.” (Ezekieli 3:26, 27) Wakati ambapo Yehova hakuwa na ujumbe wowote kwa ajili ya Israeli, Ezekieli alipaswa kuwa bubu kuhusiana na taifa hilo. Ezekieli alipaswa kusema yale ambayo Yehova alimtaka aseme wakati ambapo Yehova alimtaka aseme. Ezekieli alikuwa bubu kuhusiana na kusema maneno yenye umuhimu wa kinabii kwa Waisraeli.
Je, Tetragramatoni (zile herufi nne za jina la Mungu kwa Kiebrania) ipatikanayo katika maandishi ya Kiebrania ya Mathayo ilinakiliwa na tabibu Myahudi Shem-Tob ben Isaac Ibn Shaprut wa karne ya 14?
Kama ilivyotajwa, maandishi ya Shem-Tob ya Mathayo yatia ndani “lile Jina” ambapo kwa kweli kuna sababu nzuri kuamini kwamba Mathayo alitumia Tetragramatoni. Hivyo, tangu 1950, maandishi ya Shem-Tob yamekuwa yakitumiwa kuunga mkono kutumia jina la Mungu katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, na bado yanatajwa katika The New World Translation of the Holy Scriptures—With References.*
Je, nadhiri zinazowekwa kwa Mungu zinaweza kuvunjwa?
Yesu Kristo alisema: “Acheni tu neno lenu Ndiyo limaanishe Ndiyo, La yenu, La; kwa maana lizidilo hayo ni kutoka kwa yule mwovu.” (Mathayo 5:37) Mkristo anapaswa kuhangaikia jinsi anavyoweza kutimiza nadhiri zake kwa Mungu na vilevile kuwa mwaminifu katika mambo yote anayosema kwa Mungu na wanadamu. Namna gani akijikuta katika hali ya kutatanisha ambapo alifanya maagano na mtu mwingine ambayo hapo mwanzoni yalionekana kuwa mazuri lakini baada ya kuyachunguza zaidi yakaonekana kuwa ya kipumbavu? Hapaswi kuchukua mambo hayo kivivihivi tu. Lakini baada ya kuzungumza mambo kwa njia iliyo wazi, huenda mtu aliyefanya maagano naye akaamua kuyavunja.—Zaburi 15:4; Mithali 6:2, 3.
How many of the clean beasts did Noah take into the ark—seven of each clean beast or seven pairs of each?
What, though, of the expression “the sire and its mate” immediately after the word “sevens” at Genesis 7:2? That has led some to think that Noah was instructed to take seven pairs of every kind of clean animal. The clean beasts, however, were preserved not strictly for the purpose of procreation. Genesis 8:20 tells us that after coming out of the ark, “Noah began to build an altar to Jehovah and to take some of all the clean beasts and of all the clean flying creatures and to offer burnt offerings upon the altar.” Having on hand the seventh animal from each clean kind provided Noah with an animal for sacrifice, leaving three mated pairs for propagating their kind on the earth.
Yesu alisema: “Mkisamehe dhambi za watu wowote, zadumu wakiwa wamesamehewa hizo; msiposamehe zile za watu wowote, zadumu bila kusamehewa.” Je, maneno haya yamaanisha kwamba Wakristo waweza kusamehe dhambi?
Basi, aliyoyasema Yesu, kama ilivyorekodiwa kwenye Yohana 20:23, hayapingani na sehemu inayobaki ya Maandiko, lakini yaonyesha kwamba mitume walikuwa na mamlaka ya kipekee kuhusu msamaha, kwa kupatana na fungu lao la kipekee mwanzoni mwa kutaniko la Kikristo.
Kwa kuwa Daudi na wanaume wake walikula mikate ya toleo, je, hilo linaonyesha kwamba mtu anaweza kuvunja sheria ya Mungu chini ya hali ngumu naye asiadhibiwe?—1 Samweli 21:1-6.
Hata hivyo, hilo halimaanishi kwamba sheria ya Mungu inaweza kuvunjwa hali zinapokuwa ngumu. Kwa mfano, hali iliyoonekana kuwa mbaya ilitokea wakati mashujaa wa vita Waisraeli walipopigana na Wafilisti. Mfalme Sauli alikuwa amesema hivi: “Alaaniwe mtu yeyote atakayekula mkate kabla ya jioni na mpaka niwe nimejilipiza kisasi juu ya adui zangu!” Biblia inasema: “Siku hiyo wakaendelea kuwapiga Wafilisti.” Kwa sababu ya mapigano hayo, askari-jeshi walikuwa wamechoka nao walikuwa na njaa, ‘na watu wakaanza kuwachinja wanyama juu ya nchi, nao wakaanza kula pamoja na damu.’ (1 Samweli 14:24, 31-33) Walimtendea Yehova dhambi kwa kuvunja sheria yake kuhusu damu. Matendo yao hayakupatana na matumizi pekee ya damu ambayo Mungu alikubali, yaani, ‘kufanya upatanisho’ kwa ajili ya dhambi. (Mambo ya Walawi 17:10-12; Mwanzo 9:3, 4) Kwa rehema, Yehova alikubali dhabihu za pekee zilizotolewa kwa niaba ya wale waliotenda dhambi.—1 Samweli 14:34, 35.
Danieli alikuwa wapi wakati Waebrania watatu walipojaribiwa mbele ya sanamu kubwa iliyosimamishwa na Nebukadneza kwenye uwanda wa Dura?
Wakijaribu kueleza ni kwa nini Danieli hakuwepo, watu wengine wamesema kwamba huenda alikuwa ameenda kufanya kazi fulani ya kiserikali au alikuwa mgonjwa na hivyo hakuweza kuhudhuria. Lakini Biblia haisemi hivyo. Kwa vyovyote, Danieli alikuwa na sababu nzuri ya kutokuwepo la sivyo maafisa wa Babiloni wenye wivu wangekuwa na sababu ya kumshtaki. (Danieli 3:8) Kabla na baada ya tukio hilo, Danieli alijithibitisha kuwa mtu mwaminifu, mwenye uaminifu-mshikamanifu kwa Mungu licha ya magumu aliyokabili. (Danieli 1:8; 5:17; 6:4, 10, 11) Kwa hiyo, ingawa Biblia haisemi ni kwa nini Danieli hakuwepo kwenye uwanda wa Dura, tunaweza kuwa na uhakika kwamba alikuwa mwaminifu kabisa kwa Yehova Mungu.—Ezekieli 14:14; Waebrania 11:33.
Je, Yehova alifanya agano lake pamoja na Abrahamu huko Uru au huko Harani?
Alipokuwa akihutubia Sanhedrini, Stefano alisema hivi kuhusu Abrahamu: “Baada ya baba yake kufa, Mungu akamsababisha abadili makao yake hadi kwenye nchi hii ambamo nyinyi sasa mwakaa.” (Matendo 7:4) Maneno hayo yanaonyesha kwamba Yehova alizungumza na Abrahamu alipokuwa Harani. Ni jambo linalopatana na akili kuamini kwamba wakati huo Yehova alilitaja tena agano lake pamoja na Abrahamu kama ilivyoandikwa kwenye Mwanzo 12:1-3, kwa kuwa agano hilo lilianza kutimia Abrahamu alipohamia Kanaani. Kwa hiyo mambo yote yanapochunguzwa, tunafikia mkataa kwamba mwanzoni Yehova alifanya agano lake pamoja na Abrahamu huko Uru na huenda ikawa alilitaja tena huko Harani.
Ayubu aliteseka kwa muda gani?
wa hiyo, huenda mateso ya Yobu na kukomeshwa kwa mateso hayo kulichukua muda wa miezi michache, labda muda unaopungua mwaka mmoja. Labda unajua kwamba majaribu magumu huonekana kana kwamba yanaendelea kwa muda usio na kikomo. Hata hivyo, hatupaswi kusahau kwamba yataisha, kama yale ya Yobu. Hata majaribu tunayokabili yachukue muda mrefu kadiri gani, acheni tukumbuke utegemezo wa Mungu, kama unavyoonyeshwa katika maneno haya yaliyopuliziwa: “Maana ingawa dhiki ni ya dakika na ni nyepesi, yafanyiza kwetu utukufu ulio na uzito wenye kuzidi zaidi na zaidi na ni wa kudumu milele.” (2 Wakorintho 4:17) Mtume Petro aliandika hivi: “Mkiisha kuteseka muda kidogo, Mungu wa fadhili yote isiyostahiliwa, ambaye aliwaita nyinyi kwenye utukufu wake udumuo milele katika muungano na Kristo, yeye mwenyewe atamaliza mazoezi yenu, atawafanya imara, atawafanya kuwa wenye nguvu.”—1 Petro 5:10.